Saturday, November 19, 2016

MAKAMU WA RAIS AFURAHISHWA NA ILEMELA NA KUAMUA KUWA MLEZI







Makamu wa Rais Samia Suluhu leo amezindua Jengo la Utawala na Uzio wa Halmashauri ya Manispaa Ilemela pamoja na kugawa Madawati kwa Manispaa hiyo ikiwa ni muendelezo wa Ziara yake  Mkoani Mwanza

Katika hotuba yake kwa mamia ya Wananchi na Viongozi mbalimbali waliojitokeza kwenye Uzinduzi huo Mheshimiwa Makamu wa Rais ameeleza kuwa anafurahishwa na kasi ya utekelezaji wa shughuli za kimaendeleo ndani ya Jimbo la Ilemela na kumpongeza Mbunge wa Jimbo hilo huku akiwaasa wananchi wa Ilemela kumtumia Vizuri Mbunge huyo ambaye Pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi

'… Mna Mbunge Mzuri naamini mkimtumia vyema atawasaidia katika kuipanga Vizuri Ilemela…'
Katika kuvutiwa na Kauli mbiu ya Wilaya Ilemela inayosema kuwa ILEMELA NI YETU TUSHIRIKIANE KUIJENGA Mhe Makamu wa Rais ameongeza kuwa Maendeleo ya sehemu  huletwa na watu wa eneo lile kwa kufanya Kazi kama Kauli Mbiu ya Serikali inavyosema HAPA KAZI TU

Aidha Mhe Makamu wa Rais amesema kuwa atapendezwa iwapo Kauli Mbiu hiyo itakuwa Kauli Mbiu ya Mkoa na kuongeza kuwa atakuwa Mlezi wa Wilaya Ya Ilemela kufuatia kufurahishwa kwake na Kasi hiyo ya Utekelezaji wa Shughuli za kimaendeleo

Akimkaribisha Makamu wa Rais Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe John Mongella amemuhakikishia Makamu huyo kuwa Kasi ya Maendeleo ya Ilemela ni kubwa na kusema kuwa wasipobweteka na kuongeza Juhudi itakuwa Wilaya ya Mfano ndani ya nchi yetu

Nae Mbunge wa Jimbo hilo na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe Daktari Angeline Mabula mbali na kuwapongeza Mhe Rais na Makamu wake amemshukuru Makamu wa Rais na kuahidi kuwa kama Mteule wa Rais atahakikisha anatekelza Ilani ya Chama kama inavyoelekeza kwa kushirikiana na Wananchi kama Kauli Mbiu inavyoelekeza huku akifafanua juu ya utengenezaji wa madawati 1000 yaliyotokana na nguvu za wananchi na kumuomba kutoa msaada pale itapohitajika

'… Wewe ni Mama na Mimi ni Mama Pale tunapoomba Msaada tunakuomba utuunge Mkono…'

' Ilemela ni Yetu, Tushirikiane kuijenga'

Imetolewa Na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ilemela
18.11.2016


0 comments:

Post a Comment