Saturday, November 19, 2016

MBUNGE WA ILEMELA ALIPONGEZA KANISA KATOLIKI KWA KUSAIDIA MAENDELEO YA JAMII.












MBUNGE WA ILEMELA ALIPONGEZA KANISA KATOLIKI KWA KUSAIDIA MAENDELEO YA JAMII.

Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mhe Daktari Angeline Mabula leo ameshiriki mahafali ya Shule ya Sekondari ya Mtakatifu Maria iliyopo Nyegezi Malimbe ikiwa ni utekelezaji wa majukumu yake katika kuhakikisha anawatumikia wananchi wote na kuleta chachu ya maendeleo kwa wananchi

Akihutubia mamia ya wazazi na wanafunzi waliohudhuria mahafali hayo Mhe Mabula amelishukuru Kanisa Katoriki kwa kuisaidia Serikali katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo  huku akiwahakikishia kuwa Serikali itaendelea kutatua changamoto za Ardhi kwa taasisi mbalimbali za kidini

Aidha Mhe Angeline Mabula amewakumbusha wanafunzi wa shule hiyo kuyaishi maisha ya Seminari kwa kipindi chote cha maisha yao wakati huu wanapoondoka shuleni  na kuyaendeleza mafundisho waliyoyapata shuleni hapo

'…Seminari ni Tanuru la wito, Seminari ni sehemu ya kuzalisha wahudumu wa kanisa ni lazima kuyaishi maisha ya Seminarini huko muendako…'

Akimkaribisha Mgeni rasmi huyo Baba Askofu wa Jimbo kuu la Mwanza  Yudathadei Rwaichi amemshukuru Mbunge huyo huku akimuhakikishia juu ya shule hiyo kuendelea kutoa elimu kwa kuzingatia Masomo, Kazi, Sala na Michezo huku Mkuu wa Shule hiyo akielezea namna Seminari hiyo inavyofanya vyema Kimkoa na Kitaifa

Mahafali hiyo imehudhuriwa pia na Mh.mbunge wa jimbo la Nyamagana Mh.Stanislaus Mabula,mbunge wa Magu Mh.Kiswaga,Mh.Maria Kangoe,waheshimiwa madiwani na viongozi wa chama walioongozwa na m/kiti wa uwt mkoa wa Mwanza Mh.Hellen Bogohe

'Ilemela ni Yetu, Tushirikiane kuijenga'


Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ilemela
19.11.2016

0 comments:

Post a Comment