Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Daktari Angeline Mabula
amehitimisha mashindano ya mpira wa miguu yaliyohusisha Timu za kutoka Kata
zote zilizopo ndani ya Wilaya ya Ilemela yaliyojulikana kama Angeline Ilemela
Jimbo Cup yaliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Vyama vya Siasa na Serikali
yaliyofanyika Uwanja wa CCM Kirumba
Angeline Ilemela Jimbo Cup iliasisiwa na Mbunge
wa Jimbo la Ilemela kwa Lengo la Kukuza Vipaji mbalimbali vya Michezo
vinavyopatikana ndani ya Jimbo hilo na kuifanya Michezo kuwa Ajira na yenye
tija kwa Jamii ya Ilemela na Taifa kwa Ujumla wake
Fainali za Angeline Ilemela Jimbo Cup zilihusisha
Timu za Kata ya Bugogwa na Kata ya Ibungilo ambapo Timu ya Kata Bugogwa ilianza
kwa kuijeruhi Timu ya Kata Ibungilo kwa magoli 2 kwa 0 kabla ya
Mshambuliaji Jezi namba 11aliyejulikana kwa jina la Andrea kuipatia goli la
kwanza Timu yake mpaka Dakika 90 ya mchezo huo ikimalizika kwa Timu zote
kutoka Sare ya Magoli 3 kwa 3 na mwishowe mchezo kumalizika kwa Timu ya Bugogwa
kuigaragaza Timu ya Ibungilo kwa mikwaju ya Penati ya goli 1 kwa 0, Wakati Timu
ya Kata Kitangiri ikiibuka Mshindi wa Tatu kwa kuichapa Timu ya Kata Shibula
magoli 2 kwa 0
Akizungumza katika Mchezo huo Mbunge wa Ilemela
na muasisi wa Angeline Ilemela Jimbo Cup
Mheshimiwa Angeline Mabula amesema kuwa Uwepo wa Ligi hiyo ni Utekelezaji wa Ahadi yake alioitoa kwa Wananchi wake kipindi cha Uchaguzi katika kuhakikisha anaboresha michezo yote na kuibua Vipaji vipya vinavyopatikana ndani ya Jimbo hilo huku akiifanya Michezo kuwa Ajira
'…Hii ni Ahadi yangu ya Kipindi cha Uchaguzi katika kuibua Vipaji vipya Ilemela na kuifanya Michezo kuwa Ajira kwa Vijana wetu...'
Mheshimiwa Angeline Mabula amesema kuwa Uwepo wa Ligi hiyo ni Utekelezaji wa Ahadi yake alioitoa kwa Wananchi wake kipindi cha Uchaguzi katika kuhakikisha anaboresha michezo yote na kuibua Vipaji vipya vinavyopatikana ndani ya Jimbo hilo huku akiifanya Michezo kuwa Ajira
'…Hii ni Ahadi yangu ya Kipindi cha Uchaguzi katika kuibua Vipaji vipya Ilemela na kuifanya Michezo kuwa Ajira kwa Vijana wetu...'
Nae Waziri wa Habari na Michezo Mheshimiwa Nape
Nnauye amempongeza Mbunge wa Ilemela kwa kuasisi Ligi hiyo pamoja na hatua
mbalimbali anazochukua katika kukuza Michezo huku akiahidi kumuunga mkono mapema
mwakani itakapoanza tena Ligi hiyo
Wakati huo huo Waziri huyo ameahidi Laki
Mbili kwa kila Goli litakalofungwa kupitia fainali hizo kwa mshindi
Aidha Mshindi wa Kwanza wa Fainali hizo
alijinyakulia Kitita cha Shilingi Milioni moja, Seti Moja ya Jezi na
Kikombe huku Mshindi wa Pili akipata Kitita cha Laki Tano, Seti Moja ya Jezi na
Kikombe na Mshindi wa Tatu akiambulia Laki Tatu, Seti Moja ya Jezi na Kikombe
Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ilemela~Mwanza
0 comments:
Post a Comment